Halmashauri
ya Manispaa ya Temeke yatenga zaidi ya shilingi milioni 434 katika bajeti ya
2013/2014 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya usafi wa mazingira.
Hayo
yamesemwa naAfisa Afya Mkuu wa Manispaa ya Temeke Bw. Ernest Mamuya leo
Jijini Dar es salaam wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari, Alisema manispaa
hiyo imeweza kuendesha ukaguzi katika maeneo ya kutolea huduma kama
hoteli na katika makazi ya watu ili kuwabaini wanaochafua mazingira.
Katika
kufanikaisha suala la usafi katika manispaa hiyo vifaa vitakavyonunuliwa ni
Compactor 1,tela moja la futi 40 kwa ajili ya usafirishaji taka,ununuzi wa
mashine 3 za kusafishia barabara,kununua gari 1 la maji taka na kujenga vizimba
3 vya kuhifadhia taka kwa muda.
Ambapo
katika kuhakikisha halmashauri inaongeza kiwango cha udhibiti taka na kuboresha
hali ya usafi halmashauri imenunua malori mapya 3 aina ya TATA katika bajeti ya
2012/2013 ambayo yaligharimu milioni 324.
Bw.
Mamuya alibainisha kuwa manispaa hiyo ina mikakati mbalimbali ikiwemo
kusafisha maeneo muhimu ikiwa ni pamoja na barabara kuu,maeneo ya wazi,
masoko, mifereji na kuongeza uwezo wa kukusanya
taka,kuzihifadhi na kuzisafirisha kwenda dampo.
Alisema
kuwa Mkakati mwingine ni kuelimisha na kuhamasisha jamii ili iweze kuunga mkono
na kushiriki katika kuweka mazingira katika hali ya usafi.
Aliongeza
kuwa Halmashauri hiyo imefanikiwa kuzuia magonjwa ya milipuko kwa kipindi
cha miaka mitatu mfululizo kufuatia mikakati kabambe ya kuhamasisha na
kusimamia usafi wa Mazingira katika ngazi ya Kaya na kuigawa halmashauri hiyo
katika kanda 5 za ufuatiliji na usimamizi wa usafi wa mazingira ili kurahisisha
kazi ya ufuatiliaji na usimamizi wa usafi.
Naye
Afisa Habari wa Manispaa ya Temeke Lynn Chawala alisema Manispaa hiyo
inatarajia kubadili utaratibu wa kutupa taka dampo la
pugu na kwenda kutupa Kisarawe II ambapo ni karibu zaidi hali
itakayopunguza gharama za kusafirisha taka